HOT NEWS

    Featured Posts

Loading...

Askofu ampasulia Majaliwa jipu la polisi kuingia bungeni

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na
Moshi. Mkuu mpya wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk Fredrick Shoo jana, mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alielezea kushangazwa kwake na kile alichokiita “jeshi kuingizwa ndani ya Ukumbi wa Bunge la Jamhuri mjini Dodoma”.
Alisema hayo mjini hapa alipokuwa akitoa hotuba yake ya kwanza mara baada ya kuingizwa kazini kushika wadhifa huo atakaoutumikia kwa miaka minne.
Shoo ambaye pia ni Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, anachukua nafasi ya Askofu Dk Alex Malasusa ambaye amemaliza muda wake wa uongozi.
Hafla hiyo ambayo Majaliwa alikuwa mgeni rasmi, ilihudhuriwa pia na mawaziri wakuu wastaafu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye na maaskofu zaidi ya 28.
Akizungumza kwa hisia, Askofu Dk Shoo alionekana kuguswa na mambo matano yaliyojitokeza katika Taifa.
Polisi bungeni
Alieleza kutoridhishwa kwake na mwenendo wa Bunge, akisisitiza kuwa ni lazima mihimili mitatu ya dola ijiendeshe kwa uhuru.
“Iachiwe ifanye kazi yake kwa uhuru na kila mhimili utunze heshima hiyo. Tunasikitishwa sana na hali inayoendelea katika Bunge letu na nashukuru nimewaona baadhi ya wabunge humu,” alisema.
Wabunge waliokuwapo ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, Mbunge wa Moshi Mjini, Jaffar Michael, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema Anthony Komu wa Moshi Vijijini, James Mbatia wa Vunjo na Lazaro Nyalandu wa Singida Kaskazini.
“Hili ni lenu na Spika wenu (akiwageukia wabunge). Bunge ndiyo nyumba ya demokrasia kama kweli Tanzania tunataka kujenga jamii ya kweli ya inayoheshimu misingi ya kidemokrasia. Sisi tunatarajia kuona na kusikia hoja zikijadiliwa kwa uwazi na katika hali ya kistaarabu. Kwa kuchezeachezea heshima hii ya Bunge sasa tunaona juzijuzi tu jeshi linaingia bungeni. Nyumba ya demokrasia haiingizwi majeshi. Kwa hiyo wabunge tunzeni heshima yenu,” alisema na waumini wa kanisa hilo kumshangilia.
Utumbuaji majipu
Askofu huyo wa Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, alimpongeza Rais John Magufuli, Waziri Mkuu, Majaliwa na timu yao kwa namna walivyoanza vizuri katika utawala wa awamu ya tano.
“Rais ameshaweka wazi kwa wananchi nia yake ya kufufua uchumi na kupambana na ufisadi. Katika muda mfupi huu wa uongozi wake, mmekwishakuanza (Waziri Mkuu) kutumbua majipu makubwa ya ufisadi,” alisema na kuongeza:
“Tunamwomba sana Rais na timu yake aendelee kutumbua majipu hayo kwa ujasiri mkubwa na miji ya majipu hayo ioshwe na kukamuliwa ili yasirudie.”
Hata hivyo, alitahadharisha kuwa utumbuaji huo unatakiwa ufanyike kwa hekima na misingi ya uwazi, ili wasio na nia njema wasitumie kuwakomoa wasio na hatia.
“Yale majipu ambayo ni hasa, hayo yasiachwe kutumbuliwa na msiwe na hofu yoyote kutoka kwa watu watakaowapinga, najua kuna watu wanajipanga kuwapinga, msiwe na hofu yoyote,” alisema Askofu Shoo.
Mkwamo Zanzibar
Akizungumzia mkwamo wa kisiasa visiwani baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kufuta uchaguzi na kutangaza tarehe ya kuurudia, Askofu Shoo alisema yanayoendelea huko yanalitia doa Taifa.
“Tunamuomba pia Mungu awape hekima na ujasiri wa kushughulikia suala la Zanzibar ili maridhiano na haki itendeke na nchi yetu iendelee kuwa na utulivu na amani. Mambo yanayoendelea kule Zanzibar yasipodhibitiwa vizuri yataweza kutia doa Awamu ya Tano ya uongozi.”
Katiba mpya
Kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, Askofu Shoo alisema hayo ndiyo matarajio makubwa ya Watanzania ambao wanataka kuona Serikali ya Awamu ya Tano ikiwatimizia ndoto hiyo.
“Tunazidi kumuomba Mungu. Matarajio ya Watanzania ni uwapo wa Katiba Mpya inayoheshimu matakwa ya wengi na inayosisitiza utawala wa sheria na haki za kibinadamu,” alisema na kuongeza:
“Ninashauri mchakato wa Katiba Mpya ufikiriwe kwa upya na utumike kama njia ya kuganga madhaifu na majeraha yaliyotokea au ambayo yapo katika awamu zote zilizotangulia.”
Ada elekezi
Akizungumzia ada elekezi kwa shule za binafsi, Askofu Shoo alitaka suala hilo litizamwe upya tena kwa kuwashirikisha wadau wa elimu nchini.
“Nina imani Serikali ikiboresha shule zake hakutakuwa na haja ya kuweka ada elekezi. Tunachohitaji katika ubora wa elimu ni kuanzisha mamlaka inayojitegemea ya ithibati na udhibiti. Kuwa na mamlaka hiyo na ikijitegemea naamini kutaleta mafanikio katika ubora wa elimu.”
Waziri Mkuu
Akihutubia kwa niaba ya Rais, Majaliwa alisema wabunge wanapaswa kuwa kioo cha jamii.
“Ulipozungumzia hili ulizungumzia Bunge na mimi nashukuru umelieleza hilo la wabunge wenzangu. Jambo hilo ni letu, tutahakikisha suala la demokrasia linaimarishwa ndani ya Bunge,” alisema.
“Lakini pia nataka nieleze Bunge ni eneo ambalo linaweza kuijenga jamii hii mpya. Wabunge ni kioo, ni watu wa kuigwa. Hivyo ni vyema tukalitumia Bunge kwa lugha sahihi na tabia nzuri. Tutaendelea kusimamia lugha nzuri ndani ya Bunge ili wanaoona waweze kuiga. Niwahakikishie Watanzania tutaendelea kuzungumza na wabunge ili bungeni pawe mahali panapojenga tabia njema,” alisema.
Kuhusu Katiba Mpya, alisema hoja ya Askofu Shoo ifanyiwe kazi na akadokeza kuwa amekuwa akizungumza na wabunge juu ya suala hilo.
“Suala la ada elekezi kwa shule binafsi litazungumzwa na wadau wote ili kutoa mwelekeo sahihi. Nataka nikuahidi Baba Askofu, tutaziboresha shule zote za umma ili ziweze kutoa elimu bora,” alisema.
Askofu wa Jimbo Katoliki Moshi, Issac Aman alisema kama kuna jipu linalopaswa kutumbuliwa, basi ni la Watanzania kukosa moyo wa uzalendo.
Askofu huyo alisema ufisadi na ubinafsi unaofanywa na baadhi ya Watanzania ni matokeo ya kukosekana kwa uzalendo na uadilifu.

BAD NEWS:.. A WOMAN SIGN MERCY AFTER AN ACCIDENT IN THIS MORNING


KUTOKA MOSHI:..CHADEMA JANA IMEUWASHA MOTO HUKO MOSHI KWA WANAOSALITI CHAMA HICHO


Moshi. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeanza kuwasakama madiwani wanaodaiwa kukisaliti katika Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.
Katika uchaguzi wa meya uliofanyika Desemba 16, mwaka jana madiwani wawili wa chama hicho walidaiwa kukisaliti na kumpigia kura mgombea wa CCM, Priscus Tarimo. Hata hivyo, katika uchaguzi huo uliokuwa na wajumbe 30, mgombea wa Chadema, Raymond Mboya aliibuka kidedea kwa kupata kura 22, huku Tarimo akipata tano.
Tafsiri ya matokeo hayo ni kuwa kama madiwani wa CCM katika baraza hilo wako watatu na mgombea wao alipata kura tano, ni wazi madiwani wa Chadema walimpigia.
Wiki iliyopita Kaimu Katibu wa chama hicho katika manispaa hiyo, John Minja aliwaandikia barua madiwani wanaodaiwa kufikia watano wakituhumiwa kuhusika na usaliti huo na kutaka wajieleze.
“Baada ya kusoma taarifa ya kamati ya uchunguzi imeonekana wewe ni mmoja kati ya madiwani waliokisaliti chama wakati wa uchaguzi wa meya na naibu meya,” ilisomeka sehemu ya barua waliyopelekewa.
Barua hiyo ilitumwa kwa madiwani hao kila mmoja na nakala yake, ikidai kitendo hicho kilikiuka katiba ya chama na kanuni za madiwani wa Chadema ibara ya 5.0 vifungu vidogo vya (a) na (c).
“Kamati ya utendaji kwa mamlaka iliyonayo inaagizwa kuleta utetezi wako ndani ya siku 14 kuanzia tarehe unapopokea barua hii. Mwisho wa kupokea utetezi ni tarehe 04.02.2016,” ilisema barua hiyo. Hata hivyo, baadhi ya madiwani wanadai kuwapo kwa mpango mahususi wa kuwaondoa wasiomnyenyekea mmoja wa viongozi, jambo ambalo hawatakubali.
“Kwanza kura zilipigwa kwa siri, hivi unajuaje nani alimpigia nani? Hiki kinachofanyika ni kututisha lakini hatutabadilika na tunazijua vizuri haki zetu,”alidai mmoja wa madiwani hao.
Madiwani hao ambao waliomba majina yao yasitajwe walidai hata uamuzi wa kumsimamisha Katibu wa Chadema wa manispaa hiyo, Steven Buberwa ni mwendelezo wa kukigawa chama.
Mwenyekiti wa Chadema Manispaa ya Moshi ambaye pia ni Mbunge wa Moshi Mjini, Jaffar Michael alisema bado hawajafikia hatua za kuwachukulia hatua madiwani na kinachoendelea ni uchunguzi.

HABARI NZITO:...WATU WANAODAIWA NI MAJANGILI WATUNGUA HELKOPTA NA KUUA RUBANI

Watu wanaodaiwa kuwa ni majangili na wawindaji haramu wameitungua kwa risasi helkopta ya doria ya wanyamapori katika pori la akiba la maswa lililoko wilaya ya Meatu mkoani Simiyu kusini mwa hifadhi ya taifa ya Serengeti na kumuua rubani wa helkopita na kumjeruhi askari mmoja wa wanayamapori.
Kufuatia tukio hilo, waziri wa maliasili na utalii Profesa Jumanne Maghembe amefika katika eneo la tukio na kusisitiza kwamba serikali kwa kushirikiana na vyombo vyote vya dola na vyombo vya ulinzi na usalama inaanzisha mkakati mpya wa kupambana na ujangili na uwindaji haramu wa maliasili ikiwemo Tembo ambao ni rasilimali muhimu kwa taifa na kwa uhifadhi wa taifa la Tanzania.
Waziri Maghembe ambae amefika kwenye eneo hilo ilipotunguliwa helkopita hiyo katika safari iliyokuwa na msukosuko mingi ya barabara na hasa kipindi hiki cha mvua na kuikuta helkopita iliyokuwa inarushwa na kepten Roger Gower raia wa Uingereza ambae alifariki baada ya kujeruhiwa kwa risasi amesema tukio hilo limewakera wadau wote wa uhifadhi na serikali kwa ujumla na kamwe haliwezi kuachwa lipite bila hatua madhubuti kuchukuliwa huku akiwaonya baadhi ya watumishi wa serikali na askari wa wanyamapori wanaoshirikiana na wahalifu kuwa sasa kiama chao kimefika.
Nae kamanda wa upelelezi wa mkoa wa Simiyu Jonathan Shana amesema tukio hilo lilitokea jana jioni wakati helkopita hiyo ikiwa katika doria baada ya kusikika milio ya risasi ya majangili katika pori hilo ambapo Tembo watatu waliuwawa na kwamba watu watatu wanashikiliwa na polisi wakihojiwa kufuatia tukio hilo ambapo mkurugenzi mkuu shirika la hifadhi za taifa Tanzania Tanapa Allan Kijazi amesisistiza umuhimu wa wadau kuongeza nguvu katika kukabiliana na matatizo ya ujangili nchini.

TODAY TANZANIA NEWSPAPERS ON 31/1/2016

DSC00595    DSC00579  DSC00587DSC00589DSC00590DSC00591DSC00592DSC00593
DSC00594DSC00597DSC00598DSC00599DSC00600DSC00581DSC00582DSC00583DSC00584DSC00585DSC00586DSC00601DSC00603
UDSC00574DSC00575DSC00576DSC00577DSC00578

MBUNGE WA CHADEMA ACHANIWA SUTI YAKE NA POLISI

 Mbunge wa Jimbo la Kilombero, Peter Lijuakali akitolewa bungeni na polisi.
Na Mwandishi Wetu, Risasi Jumamosi..

DODOMA: KALI ya mwaka. Mbunge wa Jimbo la Kilombero, Peter Lijuakali wa Chadema, amechaniwa suti mbili katika matukio mawili tofauti na Jeshi la Polisi ndani ya wiki moja, Risasi Jumamosi linakutaarifu.

Mbunge wa Jimbo la Kilombero, Peter Lijuakali..

Katika tukio la kwanza, mbunge huyo alitolewa nje kwa nguvu kutoka Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero, baada ya kukaidi agizo la mwenyekiti wa kikao, Yahaya Nania la kumtaka asishiriki katika zoezi la kuapishwa kwa madiwani wateule na kumchagua mwenyekiti na makamu wa halmashauri hiyo kwa kili kilichodaiwa kuwa hakuwa mjumbe halali wa baraza hilo.

Katika purukushani hizo, zilizotokea Januari 24 mwaka huu, ambazo yeye aligoma kutoka akidai ni mwakilishi halali wa wananchi wa jimbo lake, mbunge huyo alichaniwa suti yake katika vuta nikuvute ya polisi.

Katika tukio la pili, Januari 27, mwaka huu, lililosababisha suti yake nyingine kuchanwa na polisi, Lijualikali alikuwa mmoja wa wabunge wa upinzani waliotolewa nje kwa nguvu, baada ya kukaidi amri wa Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge ya kukaa chini na kutulia.

Wabunge hao walichukuliwa hatua hiyo baada ya kupinga kujadiliwa kwa hotuba ya rais, aliyoitoa wakati wa uzinduzi wa Bunge Novemba mwaka jana, wakitaka kwanza kupata ufafanuzi wa serikali kwa kitendo chake cha kulizuia Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kurusha vipindi vyote vya vikao vya Bunge moja kwa moja (live).

Kana kwamba haitoshi, wabunge wa upinzani kwa mara nyingine walitoka nje ya Bunge katika kikao chake cha asubuhi, Alhamisi iliyopita baada ya Naibu Spika, Tulia Akson kukataa kusikiliza mwongozo uliokuwa ukiombwa na wapinzani, baada ya Naibu huyo kuzuia kujibiwa kwa swali la mmoja wao kuhusu elimu ya bure.

HABARI YA HIVI PUNDE:..(VIDEO)..RAIS MAGUFULI AFANYA KUFURU YA MWAKA KWA MKUU WA MAJESHI NCHINI "JENERALI MWAMUNYANGE" NA HII HAIJAWAHI KUTOKEA TZ, MKUU WA MAJESHI APIGWA MIAKA KADHAA NA RAIS

Rais John Pombe Magufuli amemwongeza muda wa mwaka mmoja zaidi Mkuu wa Majeshi Nchini Jenerali Davis Mwamunyange kuendelea kuongoza Jeshi. Full stori ipo kwenye hii video hapa chini



ZITTO KABWE: SERIKALI YA AWAMU YA 5 IMEANZA NA MGUU MBAYA,ISIPOJIPANGA UPYA ITAENDELEA KUAIBIKA

 

Kauli za Zitto Kabwe Asubuhi ya leo Facebook;

"Serikali ijue kuna Bunge. Bunge lina wabunge makini na wenye mapenzi ya dhati kwa Taifa letu. Serikali isipojipanga upya itaendelea kuaibika" 



"Bunge limeiamuru Serikali kuleta Mpango wa Maendeleo. Shughuli ya kwanza ya Serikali Bungeni imeondolewa kwa hoja kutoka Upinzani. Serikali ya Awamu ya 5 imeanza na mguu mbaya. Wajue Bunge lipo. Hatuburuzwi"

BREAKING NEWS:..SHAMBA LA WAZIRI MKUU STAAFU SUMAYE LILILOVAMIWA NA WANANCHI LAIBUA MAZITO TENA, SERIKALI YATOA TAMKO ZITO


WAZIRI Mkuu Mstaafu Mhe. Fredrick Sumaye, ameiangukia serikali na kuomba msaada baada ya wananchi kuchukua sheria mkononi na kuvamia eneo lake la ekari 33 lililopo Mabwepande katika Manispaa ya Kinondoni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.



Serikali imemuahikikishia Mhe. Sumaye kuwa haina mpango wa kumkandamiza mtu mnyonge wala tajiri hivyo itahakikiha inatoa haki kwa kila mmoja baada ya wiki mbili kwa kua imesikiliza pande zote mbili katika mgogoro huo. 

Akizungumza katika kikao cha pamoja kati ya wananchi wa kitongoji cha Kimondo mtaa wa mji mpya Kata ya Mabwepande na Mhe. Sumaye Dar es Salaam jana asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda alisema ili kumaliza mgogoro huo ambao Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye ameiomba serikali kuingilia kati ni lazima busara kutumika. 

Alizitaka pande hizo mbili kuiachia serikali kwa wiki mbili ili kutafuta njia bora ya kumaliza tatizo hilo huku wananchi wakitakiwa kuacha kuendelea na ujenzi na kugawiana maeneo katika shamba hilo. 

“Serikali ya Rais Magufuli ni sikivu na ndio maana ilikuwa tayari kumsikiliza Waziri Mkuu wetu Mstaafu Sumaye na kusikiliza wananchi. ili kutenda haki tunatambua migogoro ya ardhi ilivyokuwa na athari kwa jamii hatuna mpango wa kumkandamiza tajiri wala mnyonge,”alisema. 

Alisema katika eneo hilo anajua jinsi wananchi walivyotumia nguvu katika kuwekeza ujenzi na rasilimali zao lakini kwa sasa wasitishe shughuli hizo na kuendelea kugawana maeneo na Sumaye pia kuacha uwekezaji ili kutafuta suluhu. 

"Zipo njia nyingi tutazitumia kumaliza mgogoro huu ikiwemo kufuata sheria kwa kuangalia iwapo mzee wetu alikiuka taratibu za kumiliki ardhi kama ilivyodaiwa na wananchi ili tujue hatua za kuchukua,”alisema. 

Alisema pia wanaweza kukaa na Sumaye na kuzungumza naye ili kukubali hasara kwa kutoa eneo kidogo na kuwapatia wananchi hao ambao hawana makazi au Manispaa kutafuta eneo mbadala na kuwauzia kwa bei nafuu. 

Alizitaka pande hizo mbili kutambua umuhimu wa kulinda amani katika mgogoro huo kwa changamoto zilizopo kutatuliwa bila kutumia nguvu. 

Makonda pia aliagiza serikali ya kijiji kufanya utambuzi wa wananchi hao wenye makazi katika shamba la Sumaye. 

Awali katika mkutano huo Mhe. Sumaye alimueleza Mhe. Makonda jinsi serikali ilivyo na kazi ngumu ya kushughulikia migogoro ya ardhi na kuomba kutumia busara zake kumpatia eneo hilo analomiliki kihalali. 

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kama nilivyokueleza awali serikali yetu inakazi ngumu sana hasa kutokana na viongozi wa chini kutokuwa wasikivu na wakweli .Eneo hili namiliki kihalali ,nina nyaraka zote na ninalipia kila mwaka na nilikuwa katika mpango wa kutafuta wafadhili ili kuliendeleza kwa kujenga Chuo Kikuu,”alisema. 

Alisema yeye na familia yake waliuziwa eneo hilo toka mwaka 1997 na anaamini serikali itatenda haki. 

Diwani wa kata hiyo Suzan Masawe alisema anauthibitisho kuwa eneo hilo lilikuwa pori na Sumaye alilitelekeza kwa muda mrefu na kusababisha uhalifu ikiwemo wanawake kubakwa,mali za wizi kufichwa na uhalifu mbalimbali. 

Alisema kutokana na hatua hiyo walimtafuta Sumaye lakini hakuwa na ushirikiano kwakuwa hata alipofanya uwekezaji kwa kuchimba kisima cha maji alikataa kuwapa wananchi . 

Suzan alisema kutokana na hasira za wananchi hao kwa kukosa huduma za kijamii kwa muda mrefu ikiwemo eneo hilo kutokuwa na shule,Zahanati wala kituo cha polisi waliamua kuvamia na kujigawia maeneo. 

Mmoja wa wananchi hao Athuman Mnubi alikiri kweli hawana umiliki halali wa eneo hilo na katika hatua ya kutafuta makazi walivamia msitu huo uliotelekezwa na Sumaye. 

Alisema wanaamini kutokana na ahadi ya serikali ya Rais Magufuli katika kupora maeneo yaliyotelekezwa na wawekezaji watasaidiwa. 

WAKATI huo huo Makonda alisimamisha na kukamata baadhi ya malori ya kokoto na mchanga, wafanyakazi na Mwekezaji wa kigeni kutoka India Sules Waljan wanaochimba mchanga,kokoto na kifusi katika eneo la Mabwepande. 

Hatua hiyo imekuja baada ya kuona uharibifu mkubwa wa mazingira na alipowahoji wafanyakazi na Mwekezaji huyo kama wanavibali walisema hawana. 

Makonda amewafikisha watuhumiwa hao kituo cha polisi cha Wazo Hill ili kutoa maelezo ya kina na kusema kuwa serikali inatumia gharama kubwa kwa uhalibifu huo wa mazingira ambao pia unafanywa katika vyanzo vya maji na matengenezo ya madaraja yanayoharibiwa ni makubwa.

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA BALOZI NA MAKATIBU TAWALA WAPYA NA MNADHIMU MKUU WA JWTZ

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 30 Januari, 2016 amewaapisha Balozi, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania na Makatibu Tawala wawili, Ikulu Jijini Dar es salaam. 



Walioapishwa ni: 
Balozi Mahadhi Juma Maalim, ambaye anakuwa Balozi mpya wa Tanzania nchini Kuwait. 


Luteni Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, ambaye anakuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akijaza nafasi iliyoachwa wazi na Luteni Jenerali Samuel Albert Ndomba, ambaye amestaafu. Kabla ya Uteuzi huu Luteni Jenerali Mabeyo alikuwa Mkuu wa Usalama na Utambuzi wa Jeshi la wananchi Tanzania. 


Kamishna Paul Moses Chagonja, ambaye anakuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, akijaza nafasi iliyoachwa wazi Madeni Kipande ambaye uteuzi wake ulitenguliwa. 


Kamishna Clodwig Mathew Mtweve, ambaye anakuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, akijaza nafasi iliyoachwa wazi na Faisal Issa ambaye uteuzi wake ulitenguliwa. 


Akizungumza baada ya kuapishwa, Balozi Mpya wa Tanzania nchini Kuwait Mheshimiwa Mahadhi Juma Maalim, ameahidi kuiwakilisha vyema Tanzania nchini Kuwait hususani katika uchumi ili Tanzania iweze kunufaika na ushirikiano uliopo baina ya mataifa haya mawili. 


Nae Mnadhimu Mkuu wa Jeshi wa wananchi Tanzania Luteni Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, ameahidi kuendeleza kazi nzuri iliyofanywa na Mtangulizi wake Luteni Jenerali Mstaafu Samuel Albert Ndomba ya kuhakikisha anamshauri vizuri Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na hivyo kuliwezesha Jeshi hilo kutekeleza wajibu wake ipasavyo. 


Kwa upande wao, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Kamishna Clodwig Mathew Mtweve na Katibu wa Mkoa wa Katavi Kamishna Paul Moses Chagonja, wameahidi kufanya kazi kwa juhudi na maarifa katika kusukuma gurudumu la maendeleo kwenye mikoa waliyopangiwa, ikiwemo kusimamia nidhamu kwa watumishi wa umma. 


Gerson Msigwa, 
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU 
Dar es salaam 
30 Januari, 2016
Powered by Blogger.
© Copyright JAMII YETU
Back To Top